SURA YA PILI : MADA KUU 2: LUGHA NA MATUKIO YA KIJAMII NA KITAIFA
MADA NDOGO: Sikukuu, sherehe na matukio ya kitaifa nchini Rwanda
SOMO LA 7: Sikukuu, sherehe na matukio ya kitaifa katika kalenda
7.1 Kifungu kuhusu sikukuu sherehe na matukio ya kitaifa nchini Rwanda
Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, tazameni kalenda hii ya mwaka wa
2016 kisha mjadiliane kuhusu tarehe maalum za sikukuu na matukio rasmi yaKitaifa:
Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, tazameni picha hizi kisha msome
kifungu cha habari kinachofuata kuhusu sikukuu, sherehe na matukio ya
kitaifa nchini Rwanda. Baada ya kusoma kifungu, mjibu maswali ya ufahamuyanayofuata.



Maswali ya ufahamu
1. Taja sherehe ambayo husherehekewa mwanzoni mwa mwaka.
2. Taja sherehe ambayo husherehekewa mwishoni mwa mwaka.
3. Ni tukio gani ambalo huadhimishwa tarehe saba mwezi wa Aprili
nchini Rwanda?
4. Ni sherehe gani ambayo hukumbukwa tarehe moja mwezi wa Februari
nchini Rwanda?
5. Ni sherehe gani ambayo huadhimishwa tarehe moja mwezi wa Julai
nchini Rwanda?
6. Taja sherehe mbili ambazo huadhimishwa na Wakristo.
7. Taja sherehe mbili ambazo huadhimishwa na Waislamu.
8. Sherehe ya Umuganura huadhimishwa mwezi gani?9. Sherehe ya Krismasi ni sikukuu ya dini gani?
7.2 Msamiati kuhusu sikukuu nchini Rwanda
Kutokana na kifungu cha habari mlichosoma hapo awali, katika makundi ya
wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu maana ya msamiati mpya uliojitokeza
unaohusiana na sherehe na sikukuu nchini Rwanda. Kamusi ya Kiswahili inawezakutumika inapohitajika.
Kwa mfano:
serikali: mfumo au chombo chenye mamlaka ya kutawala nchi au eneofulani.
Zoezi la 7.1
A. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni maana
ya msamiati uliopigiwa mistari katika sentensi hizi. Tumieni kamusi
panapohitajika.
1.Wanyarwanda walipigana dhidi ya wakoloni.
2.Wananchi hawafai kutumia mabavu wanapotafuta mali.
3.Nchi yetu ilipata ukombozi miaka mingi iliyopita.
4.Serikali yetu ina viongozi wazuri.
5.Utawala wa rais wetu ni wa kuigwa na viongozi wengi duniani.
B. Katika makundi yenu, tungeni sentensi sahihi kwa kutumia manenoyaliyopigiwa mistari katika sentensi za zoezi la 1A.
Zoezi la 7.2
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jazeni nafasi zilizo wazi katikasentensi hizi kwa jibu sahihi kutoka katika mabano.
1. Sherehe za mwaka mpya ________________ mwanzoni mwa kila
mwaka. (huathimishwa, huadhimishwa)
2. Rwanda ni ____________________ inayopendwa na watu wengi
ulimwenguni. (inchi, nchi)
3. ____________ ya Krismasi hufanyika tarehe 25 mwezi wa Disemba.
(Shehere, Sherehe)
4. Siku ya ______________ husherehekewa tarehe 1 mwezi wa Februari.
(washujaa, mashujaa)
5. ______________ husherehekewa wiki ya kwanza mwezi wa Agosti.(Umagunura, Umuganura)
7.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mjadili kuhusu
sherehe na sikukuu nchini Rwanda. Waeleze wenzako:
1. Shughuli zote zinazofanyika katika sherehe za mwaka mpya.
2. Nguo unazopenda kuvaa unapoenda katika sherehe za harusi.
3. Sikukuu unayopenda kuadhimisha katika kalenda. Toa sababu.
4. Umuhimu wa sikukuu na sherehe mbalimbali kwa Wanyarwanda.5. Umuhimu wa kuwa na Kalenda rasmi nyumbani.
7.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni na muigize mchezo mfupi
kuhusu sikukuu nchini Rwanda. Mwanafunzi mmoja amuulize mwenzake maswalimbele ya darasa, naye ajibu vizuri.
Mfano wa mazungumzo:
Kamana: Habari dada Mukamana.
Mukamana: Salama kaka.
Kamana: Sikukuu ya Uhuru huadhimishwa lini?
Mukamana: Sikukuu ya Uhuru huadhimishwa tarehe mosi mwezi wa Julai
kila mwaka.Kamana: Ooh! Nimekumbuka. Asante sana dada
Zoezi la imla
Funga kitabu chako kisha ufungue daftari lako na uandike kwa usahihimaneno au vifungu vya maneno ambayo mwalimu wako atakusomea.
7.5 Sarufi: Matumizi ya wakati uliopita
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni michoro hii ya masimulizi
mafupi yafuatayo kisha kila mmoja awasimulie wenzake alivyosherehekea mwakampya uliopita.

Katika sherehe za mwaka mpya uliopita, niliamka mapema, nikaoga,
nikapiga mswaki, nikavaa nguo mpya na kunywa kiamshakinywa. Baadaye
niliondoka na kuelekea kijijini kumtembelea kaka yangu. Nilipofika huko
kijijini, niliwaona watoto wengi wakicheza kandanda katika uwanja mdogo.
Nilijiunga nao. Baada ya dakika chache, mwamuzi wa mchezo huo alipuliza
kipenga cha kuashiria mwisho wa mchezo huo. Timu ya Mashujaa ilipataushindi wa mabao matatu kwa moja dhidi ya timu ya Simba.
Swali: Eleza wakati uliotumika katika masimulizi mliyosoma hapo juu pamojana masimulizi yenu kwa kutoa mifano ya vitenzi vilivyotumika.
Zoezi la 7.3
A. Orodhesha vitenzi vyote vilivyotumika katika masimulizi mliyoyasoma
hapo awali.B. Tambua nyakati zilizotumika katika vitenzi mlivyoorodhesha
Maelezo muhimu!
Funga kitabu chako kisha ufungue daftari lako na uandike kwa usahihimaneno au vifungu vya maneno ambayo mwalimu wako atakusomea.
7.5 Sarufi: Matumizi ya wakati uliopita
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni michoro hii ya masimulizi
mafupi yafuatayo kisha kila mmoja awasimulie wenzake alivyosherehekea mwakampya uliopita.
Swali: Eleza wakati uliotumika katika masimulizi mliyosoma hapo juu pamoja

na masimulizi yenu kwa kutoa mifano ya vitenzi vilivyotumika.
Zoezi la 7.3
A. Orodhesha vitenzi vyote vilivyotumika katika masimulizi mliyoyasoma
hapo awali.B. Tambua nyakati zilizotumika katika vitenzi mlivyoorodhesha.
Maelezo muhimu!
Wakati uliopita huonyesha matukio ambayo huwa tayari yameshatendeka.
Wakati uliopita hutumia kiambishi cha wakati -li-. Kiambishi hiki hutumika
katika nafsi zote za Kiswahili.
Kiambishi -ka- hutumika katika sentensi iliyo na matukio yanayofuatanakatika wakati uliopita.
Mifano:
1. Nilitembea pamoja na kakangu.
2. Aliamka akavaa nguo za michezo.
3. Mimi nilipika chakula, nikala na kulala.
4. Dereva aliwasha gari, akaliendesha haraka na kushikwa na polisi.
5. Sisi tulivuna mahindi wiki iliyopita.
Katika masimulizi ya wakati uliopita, maneno kama vile: halafu, kisha nabaadaye hutumika.
Zoezi la 7.4
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jazeni nafasi zilizo wazi katikasentensi zinazofuata kwa kutumia wakati uliopita.
Kwa mfano: Mama __________ (fua) nguo, __________ (pika) na
________ (fagia) nyumba.
Jibu: Mama alifua nguo, akapika na kufagia nyumba.
1. Kaka __________ (oga), __________ (piga) nguo pasi na _________
(enda) shuleni.
2. Mtoto __________ (kunywa) maziwa, __________ (bembelezwa) na
__________ (lala).
3. Mwanafunzi ____________ (enda) shuleni, ____________ (soma) na
__________ (fanya) mtihani.
4. Ng’ombe ____________ (kula) nyasi, ____________ (kunywa) maji
na __________ (rudi) zizini.
5. Mmea _____________ (pandwa), ____________ (wekewa) mboleana __________ (nyunyiziwa) maji.
Zoezi la 7.5
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, badilisheni sentensi hizi ziwe
katika wakati uliopita.
1. Mama anapika wali.
2. Mimi nitaenda shule.
3. Kwa nini unalia?
4. Siku ya sherehe ya Krismasi imefika.5. Wanyarwanda wanaadhimisha siku ya Mashujaa.
Zoezi la 7.6
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mtunge sentensitano sahihi kwa kutumia wakati uliopita ukitanguliza msamiati ufuatao.
Kwa mfano: Tarehe
Tarehe moja mwezi wa Februari tuliadhimisha sikukuu ya Mashujaa.
1. Uhuru
2. Ukombozi
3. Ukoloni
4. Utawala5. Siasa
7.6 Sarufi: Matumizi ya wakati ujao
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tazameni mchoro wa kifungu
kifuatacho kisha kila mmoja asimulie anavyopanga kusherehekea mwaka mpyaujao baada ya kusoma kifungu mlichopewa kwenye ukurasa unaofuata.

Swali: Eleza wakati uliotumika katika masimulizi mliyosoma hapo juu pamoja
na masimulizi yenu kwa kutoa mifano ya vitenzi vilivyotumika.
Zoezi la 7.7
A. Orodhesha vitenzi vyote vilivyotumika katika masimulizi mliyoyasoma
hapo awali.B. Tambua nyakati zilizotumika katika vitenzi mlivyoorodhesha.
Zoezi la 7.8
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, jazeni nafasi zilizo wazi kwavitenzi vilivyo kwenye mabano katika wakati ujao.
Katika sherehe za Pasaka za mwaka ujao, Kamana ____________ (enda)
kanisani kwa ajili ya ibada. Baadaye, __________ (tembelea) marafiki
zake na kusherehekea pamoja nao. Kisha jioni ________________ (rudi)
nyumbani. Ndugu yake Yusufu ______________ (pokea) kwenye kituo
cha basi. Halafu ____________ (enda) nyumbani pamoja.
Zoezi la 7.9
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni aya moja sahihi yenyekuhusisha matukio ya wakati ujao.
Zoezi la 7.10
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, badilisheni sentensi zinazofuataziwe katika wakati ujao.
Kwa mfano: Mwalimu anaandika ubaoni.
Jibu: Mwalimu ataandika ubaoni.
1. Mwanafunzi huyu anasoma kitabu cha hadithi.
2. Mbuga hii ilifunguliwa na rais wetu.
3. Darasa letu limesafishwa na wanafunzi hawa.
4. Kwa nini mnanunua vitabu vingine?5. Wanyamapori hawa wanakula nyasi.
Maelezo muhimu!
Wakati ujao hutumiwa kuonyesha matukio ambayo huwa yanatarajiwa
kutendeka. Wakati huu hutumia kiambishi -ta-. Kiambishi hiki hutumikakatika nafsi zote za Kiswahili.
Mifano:
1. Nitaomba walinzi wa mbuga waniongoze na baadaye nitapiga picha.
2. Nitavaa kanzu nzuri halafu nitaenda msikitini kusali.
3. Mwalimu atatufundisha kesho kisha atatupa mtihani.
4. Sherehe ya Idi ul Fitri itaadhimishwa mwezi ujao.
5. Wanafunzi watafanya mtihani wiki ijayo.
Katika masimulizi ya matukio ya wakati ujao, maneno kama vile: kisha,halafu, mwishowe na baadaye hutumika.
SOMO LA 8: Maadhimisho mbalimbali nchini Rwanda
8.1 Shairi kuhusu maadhimisho mbalimbali nchini Rwanda
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mtazame picha hizina hapo baadaye msome na kukariri shairi lifuatalo na kulijadili:



Maswali ya tathmini
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini na mjibu maswali haya ya
tathmini kuhusiana na shairi mlilosoma hapo awali.
1. Taja sherehe ambayo huadhimishwa mwanzoni mwa kila mwaka.
2. Sikukuuu ya Mashujaa husherehekewa lini?
3. Pasaka huadhimishwa na watu gani? Wao hukumbuka nini katika siku hii?
4. Taja sikukuu za Waislamu kutokana na shairi ulilosoma?
5. Sikukuu ya Uhuru nchini Rwanda husherehekewa lini?
6. Kumbukumbu za mauaji ya kimbari dhidi ya Watutsi hufanyika lini?
7. Shairi hili lina mishororo mingapi?
8. Taja kibwagizo cha shairi hili.
9. Sherehe za Krismasi huadhimishwa lini?10. Sikukuu ya Umuganura hufanyika lini?
8.2 Msamiati kuhusu maadhimisho mbalimbali
Kutokana na shairi mlilosoma hapo awali, katika makundi ya wanafunzi
watatu watatu, jadilini maana ya msamiati mpya uliojitokeza unaohusiana na
maadhimisho mbalimbali nchini Rwanda. Kamusi ya Kiswahili inaweza kutumikainapohitajika.
Kwa mfano:
Ukombozi: matendo au vita vya kuokoa watu kutoka kwenye hali mbayayenye mateso au hali ya unyonge.
Zoezi la 8.1
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mtunge sentensi
sahihi kwa kutumia msamiati uliopigiwa mistari katika sentensi zinazofuata.
1. Leo tunaadhimisha sikukuu ya Mashujaa.
2. Hii ni kalenda ya mwaka wa 2017.
3. Mwezi wa kwanza katika kalenda ya mwaka ni Januari.
4. Wakristo husherehekea sikukuu ya Pasaka kila mwaka.
5. Waislamu husali mara tano kwa siku.
6. Waislamu huadhimisha sherehe ya Idi-ul-Fitr kila mwaka.
7. Msimu wa sherehe za Krismasi umefika.
8. Wanyarwanda huadhimisha sikukuu ya Uhuru wa Taifa kila mwaka.
9. Leo ni tarehe kumi mwezi Disemba mwaka 2016.10. Sherehe ya Umuganura itaadhimishwa kesho
8.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mjadiliane na
kuelezana kuhusu:
1. Shughuli zinazofanyika nyumbani kwenu wakati wa sherehe za mwaka
mpya.
2. Namna mnavyoadhimisha sikukuu iliyo katika mwezi Julai.
3. Shughuli zinazotekelezwa kwenu wakati wa sherehe za Umuganura.
4. Shughuli zinazotekelezwa wakati wa kuadhimisha sikukuu ya Ukombozi
wa Taifa.
5. Shughuli zinazofanyika wakati wa kuadhimisha sikukuu ya Uhuru waTaifa.
8.4 Kusikiliza na kuzungumza: Zoezi la mazungumzo
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni mazungumzo mafupiyafuatayo na majibu yatolewe palipo na maswali mbele ya wanafunzi wenzenu.
Mazungumzo kati ya Kamana na Teta:
Kamana: Sikukuu ya Uhuru huadhimishwa tarehe gani?
Teta: Sikukuu ya Uhuru huadhimishwa tarehe moja mwezi wa Julai kila
mwaka.
Kamana: Sikukuu ya sherehe za mwaka mpya huadhimishwa tarehe gani?
Teta: Sherehe za mwaka mpya huadhimishwa tarehe moja mwezi wa
Januari kila mwaka.Endelezeni mazungumzo haya kwa maneno yenu wenyewe.
8.5 Sarufi: Vitenzi vya silabi moja
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi wawili wawili kisha mbainishe vitenzivilivyo katika sentensi hizi zenye michoro.


Zoezi la 8.2
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tungeni sentensi tano sahihi kwa
kutumia vitenzi vifuatavyo.
Kwa mfano: kuja
Jibu: Mwalimu alikuja kututembelea nyumbani kwetu.
1. kufa
2. kunywa
3. kula
4. kuwa5. kuja
Maelezo muhimu!
Katika lugha ya Kiswahili kuna vitenzi vyenye silabi moja. Vitenzi hivi
huambatanishwa na ‘ku-’ katika matumizi.
Kwa mfano:
kufa: –f
kuwa: -w
kunywa: -nyw
kula: -l
kuja: -j
Matumizi katika sentensi
1. Mtoto alikunywa dawa.
2. Ng’ombe alikula nyasi.3. Nyanya alikuja dukani.
Zoezi la 8.3
A. Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, rekebisheni sentensi hizi:
1. Mwalimu alija darasani.
2. Mbuzi wetu alifa jana.
3. Kalisa alinywa maji.
4. Dada alila wali.
5. Mama aliwa mgonjwa.B. Kanusha sentensi mlizosahihisha katika A hapo juu.
8.5.1 Vitenzi vya silabi moja, tungo yakinishi na kanushi
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni sentensi hizi kisha
mjadili ugunduzi wenu.
1. Mtoto alikunywa dawa. - Mtoto hakunywa dawa.
2. Paka wao alikufa jana. - Paka wao hakufa jana.3. Mgeni alikuja haraka. - Mgeni hakuja haraka.
Maelezo muhimu!
Vitenzi vya silabi moja huambatanishwa na ‘ku-’ katika hali yakinishi.
Katika hali kanushi, vitenzi hivi huambatanishwa na kikanushi ‘ha-’ nanafsi husika.
Kwa mfano:
1. Wagonjwa walikula chakula. - Wagonjwa hawakula chakula.
2. Walimu walikunywa chai. - Walimu hawakunywa chai.3. Paka wa jirani walikufa jana. - Paka wa jirani hawakufa jana.
Zoezi la makundi
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, chunguzeni mifano ya sentensikatika jedwali hili.

Zoezi la 8.4
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tumieni vitenzi vyenye silabi
moja vifuatavyo katika wakati uliopita hali yakinishi katika umoja na wingi.Tumieni nafsi zote za Kiswahili.
Mfano: kunywa: -nyw
Jibu: Mtoto alikunywa maziwa. - Watoto wali kunywa maziwa.
1. kuwa
2. kuja
3. kufa4. kula
Zoezi la 8.5
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tumieni vitenzi vyenye silabi
moja vifuatavyo katika wakati uliopita hali kanushi. Tumieni nafsi zote za
Kiswahili.
Mfano: kunywa: -nyw
Jibu: Mtoto hakunywa maziwa yote.
1. kuwa
2. kuja
3. kufa4. kula
Zoezi la 8.6
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, andikeni sentensi zifuatazo
katika umoja au wingi.
Kwa mfano:
Umoja: Mwalimu alikuwa darasani.
Wingi: Walimu walikuwa madarasani.
1. Mtu huyu alikuja jana jioni.
2. Wanafunzi hawa wanakunywa maziwa.
3. Mtoto anakula mkate.
4. Panya alikufa mtegoni.5. Viongozi walikuwa mjini Kigali.
SOMO LA 9: Matumizi ya kalenda ya mwaka
9.1 Mazungumzo kuhusu matumizi ya kalenda ya mwaka
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, tazameni kalenda hii ya mwaka wa
2017 kisha msome mazungumzo yaliyo hapo chini na hatimaye mjibu maswaliyanayofuata.



Maswali ya ufahamu
1. Mwezi wa Januari una Jumapili ngapi?
2. Tarehe 5 mwezi wa Mei ni siku gani?
3. Mwaka wa 2017 una siku ngapi?
4. Mwezi wa Septemba una Jumatano ngapi?
5. Sikukuu ya Mashujaa wa Taifa iliadhimishwa siku gani katika kalenda
iliyo hapo juu?
6. Krismasi itaadhimishwa siku gani katika kalenda iliyo hapo juu?
7. Sikukuu ya mwaka mpya 2017 iliadhimishwa siku na tarehe gani?
8. Mwezi wa Agosti una siku ngapi?
9. Mwezi wa Disemba una Alhamisi ngapi?
10. Ni miezi mingapi isiyokuwa na sikukuu katika kalenda iliyo hapo juu?Itaje.
9.2 Msamiati kuhusu kalenda ya mwaka
Zoezi la 9.1
(i) Kutokana na mazungumzo kuhusu matumizi ya kalenda ya mwaka
mliyoyasoma hapo awali, katika makundi ya wanafunzi watatu watatu,
jadilini kuhusu maana ya msamiati uliopigiwa mistari katika sentensi
zinazofuata. Kamusi ya Kiswahili inaweza kutumika inapohitajika.
1. Jumamosi ni siku inayotangulia Jumapili.
2. Huu ni mwezi wa Ramadhani.
3. Siku hii imekuwa ya mikutano mingi.
4. Mwezi wa kwanza katika kalenda ya mwaka ni Januari.
5. Mwaka ujao tutazuru nchi ya Kenya.
6. Sherehe za Krismasi hufanyika mwezi wa Disemba.
7. Tarehe mbili mwezi ujao tutasafiri kuelekea kijijini kwetu.
8. Tutafungua shule mwezi Mei.
(ii) Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwakutumia msamiati uliopigiwa mistari katika Zoezi la 1 (i) hapo juu.
9.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mtazame mchoroufuatao wa kalenda ya mwaka wa 2017 na kuijadili.
Katika makundi yenu, jadilini kuhusu namna ya kuisoma kalenda hiyo ya mwaka
wa 2017 na kuielewa kimatumizi. Waelezee wenzako:1. Miezi yote iliyo na siku thelathini.
2. Miezi yote iliyo na siku thelathini na moja.
3. Mwezi ulio na siku chache kuliko miezi mingine.
4. Miezi iliyo na Jumapili nyingi kuliko mingine.
5. Miezi iliyo na sikukuu au matukio rasmi ya kitaifa ya kusherehekewa.
6. Mwezi wa Disemba una Jumapili ngapi?
7. Tarehe ya kwanza katika mwezi wa Septemba ni siku gani?8. Tarehe kumi mwezi wa Agosti ni siku gani?
Maelezo muhimu!
• Kalenda ni kifaa kinachoonyesha siku, tarehe na miezi katika mwaka.
• Mwaka una miezi kumi na miwili ambayo ni: Januari, Februari,
Machi, Aprili, Mei, Juni, Julai, Agosti, Septemba, Oktoba,
Novemba na Disemba.
• Siku katika kila mwezi huanzia Jumapili hadi Jumamosi.
• Mwaka mmoja una wiki hamsini na mbili.
• Wiki moja ina siku saba ambazo ni: Jumapili, Jumatatu, Jumanne,
Jumatano, Alhamisi, Ijumaa na Jumamosi.
• Katika kalenda, siku za Jumapili huandikwa kwa kutumia wino wa
rangi tofauti.
• Siku za matukio makuu ya sherehe za kitaifa na kijamii huandikwakwa kutumia wino wa rangi tofauti.
9.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi wawili wawili kisha mwigize mazungumzo
mliyoyasoma hapo awali kati ya Birasa na Kalisa kuhusu matumizi ya kalenda yamwaka.
9.5 Sarufi
Matumizi ya herufi kubwa na alama za uandishi
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, someni kifungu kifuatacho kisha
mbainishe maneno yote yaliyotumia herufi kubwa pamoja na alama mbalimbaliza uandishi na hapo baadaye mjibu maswali ya tathmini yanayofuata.
Maswali ya tathmini
1. Eleza matumizi mbalimbali ya herufi kubwa kutokana na kifungu kifupi
mlichosoma hapo awali kumhusu Biruta.
Kwa mfano: Biruta anaishi Gikondo.
Matumizi: Herufi kubwa imetumika mwanzoni mwa jina la mtu
(Biruta) na jina la mahali (Gikondo).
2. Eleza matumizi mbalimbali ya alama nyingine za uandishi kutokana na
kifungu mlichosoma hapo juu kisha mwonyeshe matumizi katika sentensi.
Kwa mfano: Nukta (.)
Matumizi: Nukta imetumika mwishoni mwa sentensi kamili.
Mfano wa sentensi: Biruta ni mwalimu mkuu katika shule yasekondari ya Kamashashi iliyo mjini Kigali.
Zoezi la 9.2
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, rekebisheni sentensi zifuatazo
kwa kutumia alama za uandishi kwa usahihi.
Kwa mfano: neza ataenda shule jumatatu
Jibu: Neza ataenda shule Jumatatu.
1. kwa nini ulichelewa shuleni
2. lo umebeba mzigo huo pekee yako
3. mama alienda sokoni kununua ndizi machungwa viazi na nanasi
4. paka amekunywa maziwa5. ngabo atakuja lini
Zoezi la 9.3
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, rekebisheni kifungu hiki kwa
kutumia alama za uandishi pamoja na herufi kubwa kwa usahihi.
siku moja nilienda sokoni kununua ndizi sukari samaki mboga na
machungwa. njiani nilikutana na rafiki yangu birasa. alishangaa kuniona
na kusema ah kumbe wewe pia huja sokoni nikamjibu kuwa mimi hupenda
kumsaidia mama kununua bidhaa mbalimbali. nilimuuliza umekujakununua nini. akanijibu kuwa alikuja kununua mboga na samaki
Tathmini ya mada ya 2
Zoezi la 1
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mjadili maswali
yafuatayo. Waelezee wenzako kuhusu:
1. Shughuli zinazofanyika wakati wa sikukuu ya Pasaka kwa Wakristo.
2. Shughuli zinazofanyika wakati wa sikukuu ya Idi ul Fitri kwa Waislamu.
3. Shughuli na burudani zinazofanyika katika sherehe ya harusi.
4. Sherehe ya Kiislamu ya Idi ul Adha huadhimishwa lini? Jadili shughuli
zinazofanyika wakati wa sherehe hiyo.
5. Sherehe ya Kikristo ya Krismasi huadhimishwa lini? Jadili shughulizinazofanyika wakati wa sherehe hiyo.
Zoezi la 2
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, rekebisheni sentensi zifuatazo
kwa kutumia alama za uandishi kwa usahihi
kwa kutumia alama za uandishi kwa usahihi
Kwa mfano: pasaka iliadhimishwa tarehe gani
Jibu: Pasaka iliadhimishwa tarehe gani?
1. baadhi ya sherehe katika kalenda yetu ni pasaka krismasi na umuganura
2. siku ya kwanza ya wiki ni jumapili katika kalenda ya mwaka
3. kamana anaishi wapi
4. lo simu yangu imeanguka majini5. kilo moja ya chumvi huuzwa faranga mia mbili 200
Zoezi la 3
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, andikeni sentensi zifuatazo
katika wakati ujao.
Kwa mfano: Baba alinunua maji, soda na mkate.
Jibu: Baba atanunua maji, soda na mkate.
1. Mwalimu alitufundisha Hisabati.
2. Ng’ombe alikunywa maji mengi.
3. Babu alitusimulia hadithi nzuri.
4. Sikukuu ya Krismasi iliadhimishwa kwa sherehe kubwa.5. Manzi alinunua vitabu na kalamu.
Zoezi la 4
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi kwa kutumia
vitenzi vya silabi moja vifuatavyo katika wakati uliopita hali kanushi.
Kwa mfano: kuja
Jibu: Mwalimu hakuja shuleni jana.
1. kunywa
2. kula
3. kuwa
4. kuja5. kufa
Zoezi la 5
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tajeni majina ya alama zauandishi zifuatazo kisha mtunge sentensi moja kwa kila alama.
Kwa mfano: .
Jibu: Nukta
Sentensi: Tutaadhimisha sikukuu ya Ukombozi mwezi Julai.
1. ?
2. !
3. ,
4. :
5.6. ’
Zoezi la 6
Katika makundi ya wanafunzi watano watano, wasimulie wenzako kuhususikukuu yoyote mliyoadhimisha kwa kuzingatia wakati uliopita.
Zoezi la 7
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwa
kutumia vitenzi vifuatavyo katika hali yakinishi na hali kanushi kwa kuzingatiawakati ujao.
Kwa mfano: andika
Jibu: (Yakinishi): Mwanafunzi ataandika ubaoni.
(Kanushi): Mwanafunzi hataandika ubaoni.
1. sherehekea
2. kula
3. adhimisha
4. kunywa5. soma
Zoezi la 8
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, rekebisheni kifungu hiki kwa
kutumia alama za uandishi pamoja na herufi kubwa kwa usahihi.
sikukuu ya mwaka mpya huadhimishwa tarehe moja januari siku ya
mashujaa huadhimishwa tarehe moja mwezi februari je wewe uliadhimisha
sikukuu ya mwaka mpya kwa njia gani waislamu wana sherehe mbili kuu
ambazo ni idi ul fitri pamoja na idi ul adha Wakristo vilevile wana sherehe
mbili kuu ambazo ni krismasi pamoja na pasaka je wewe husherehekeasikukuu gani ya kidini.
Zoezi la 9
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu,
rekebisheni sentensi hizi kwa kutumia alamaza uandishi pamoja na herufi kubwa kwa usahihi.
1. rais aliongoza sherehe ya siku ya uhuru katika uwanja wa gikondo
2. je wewe ulihudhuria sherehe ya umuganura mwaka jana3. lo sikujua unaweza kuimba vizuri hivyo kwenye sherehe hiyo

