Topic 5
MADA KUU 5: LUGHA NA TEKNOLOJIA
Mada Ndogo: Kiswahili katika teknolojia ya habari namawasiliano.
SOMO LA 17: Simu ya mkononi
17.1 Mazungumzo kuhusu matumizi ya simu ya mkononi
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni picha zifuatazo
kisha mwelezane vifaa mnavyoona pamoja na matumizi na umuhimu wake.
Baadaye, msome kifungu cha mazungumzo kilicho hapo chini na mjibu maswaliyanayofuata.

Maswali ya ufahamu

Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu cha
mazungumzo yaliyo hapo juu kisha mjibu maswali yanayofuata.
1. Taja wazungumzaji katika kifungu cha mazungumzo ulichosoma hapo
juu.
2. Bila shaka mazungumzo yanahusiana na teknolojia. Kwa nini? Eleza.
3. Taja chombo cha mawasiliano kilichozungumziwa.
4. Orodhesha matumizi yoyote mawili ya simu ya mkononi waliyotaja
wazungumzaji.
5. Mama ana matatizo gani kuhusiana na simu yake mpya?
6. Kulingana na baba, ni mambo gani ambayo huathiri matumizi ya simu ya
mkononi kijijini kwao?
7. Teknolojia ni nini? Eleza kwa maneno yako mwenyewe.
8. Taja msamiati wa adabu ambao umetumika katika kifungu chamazungumzo mliyoyasoma.
17.2 Msamiati kuhusu simu ya mkononi
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya kutoka
katika kifungu cha mazungumzo mlichosoma na kuueleza. Zingatieni matumizi
ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale inapohitajika.
Zoezi la 17.1
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zifuatazo
kisha mtunge sentensi sahihi kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mstari.
1. Simu ya mkononi ambayo mama alinunuliwa inamsaidia sana.
2. Teknolojia katika nchi yetu imekua kwa kiwango kikubwa.
3. Simu ya babu yangu ni ya kubofya vidude.
4. Dada yangu aliye ng’ambo alinitumia arafa kwenye simu yangu.
5. Baba atampigia mwalimu wetu simu ili kuniombea ruhusa.
6. Simu mpya aliyonayo ni ya kugusa kwenye kiwambo chake.
7. Simu yangu ina kamera nzuri sana.8. Intaneti ni muhimu sana katika matumizi ya simu.
Zoezi la 17.2
Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, kamilisheni sentensi zifuatazo
kwa kutumia maneno yafuatayo:
arafa, watisapu, kunasia mawimbi, fesibuku, simu, chaji
Kwa mfano: Baba alinunua ____________ mpya baada ya ile ya
kwanza kuibwa.
Jibu: Baba alinunua simu mpya baada ya ile ya kwanza kuibwa.
1. Sharti simu iwe na ______________ ili iweze kutumika.
2. Watu wengi siku hizi wanatumia _____________ na ______________
kuwasiliana.
3. Mitambo ya ____________ katika kijiji chetu imeharibika.
4. Kaka alinitumia __________________ kunijulisha kuhusu gari jipya
alilonunua.
17.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni mchoro na picha
zifuatazo kisha mwelezane kinachoendelea kwa kurejelea:
i) Vifaa vya mawasiliano unavyoviona;
ii) Matumizi ya kila kifaa cha mawasiliano unachokiona;
iii) Umuhimu wa kila kifaa cha mawasiliano unachokiona;
iv) Kasoro au udhaifu wa kila kifaa cha mawasiliano unachokiona.
Maelezo muhimu!
Kifaa cha kutuma taarifa kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia simu
huitwa faksi. Taarifa inayotumwa pia huitwa faksi. Huhusisha matumizi
ya umeme. Faksi ni aina ya barua au ujumbe unaotumwa kwa njia ya
mashine inayoitwa faksi. Maelezo machache yanayofafanua ujumbe
pekee hutumika.
17.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, igizeni mazungumzo mliyosoma
hapo juu kati ya Baba na Mama.
17.5 Sarufi
Hali ya kuomba, tungo yakinishi
A. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
kisha mwelezane ugunduzi wenu na baadaye mjibu zoezi l7.3 linalofuata.
1. Tafadhali nipigie simu unapofika nyumbani.
2. Tafadhali imba wimbo wa taifa.
3. Tafadhali cheza mpira wa miguu.
4. Tafadhali pikeni mihogo kwa kuku.
5. Tafadhali zungumza lugha ya Kiswahili sanifu pekee.B. Badilisheni sentensi mlizosoma hapo juu kwa kutumia ‘naomba’.
Maelezo muhimu!
Msamiati wa adabu ambao hutumika kuomba mtu akutendee hisanifulani ni kama vile: tafadhali, naomba, n.k.
Zoezi la 17.3
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi tano sahihikatika hali ya kuomba, wakati uliopo.
SOMO LA 18: Matumizi ya tarakilishi
18.1 Kifungu kuhusu matumizi ya tarakilishi
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu mnachokiona
katika mchoro na picha ifuatayo na mwelezane maana na matumizi yake.
Baada ya hapo, msome kifungu cha habari kilicho hapo chini na mjibu maswaliyanayofuata.


Maswali ya ufahamu

1. Taja faida zozote mbili za mradi wa tarakilishi kwa wanafunzi.
2. Taja faida zozote mbili za tarakilishi kwa watu kwa ujumla.
3. Jina jingine la tarakilishi ni lipi?
4. Mtandao hufanya ulimwengu kuwa kama kijiji kimoja. Kweli au la? Kivipi?
Eleza.
5. Jadili upungufu mkubwa wa watisapu kulingana na kifungu ulichosoma.
6. Pendekeza anwani nyingine mwafaka kwa taarifa hii.
7. Je, teknolojia ina manufaa gani kwa nchi? Taja manufaa matano.
8. Eleza madhara yanayoweza kusababishwa na tarakilishi.
9. Matumizi ya tarakilishi yanawezesha vipi utangamano wa wanajamii
mbalimbali?
10. Jadili matumizi, umuhimu na madhara ya:a) Fesibuku b) Watisapu ch) Barua pepe
18.2 Msamiati kuhusu matumizi ya tarakilishi
Jipangeni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mtafute maana
ya msamiati mpya katika kifungu mlichosoma hapo awali. Tafuteni maana ya
msamiati huo kulingana na matumizi yake katika kifungu hicho. Tumieni kamusipale inapohitajika.
Zoezi la 18.1
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi hizi kisha
mtunge sentensi zenu kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mistari.
1. Teknolojia imeufanya ulimwengu kuwa kama kijiji kidogo.
2. Tarakilishi ina manufaa mengi kwa binadamu.
3. Mtandao humwezesha mtafiti kupata taarifa nyingi.
4. Mradi wa tarakilishi kwa kila mwanafunzi utafaulu.
5. Mimi huisoma kamusi ya Kiswahili kwenye tarakilishi.
6. Tunaweza kuzifahamu tamaduni za jamii jirani kupitia kwa mtandao.
7. Wanajamii mbalimbali hutangamana kupitia kwa mtandao.
8. Akaunti yangu ya fesibuku imefungwa.
9. Watisapu yangu imejaa picha tele za harusi ya kaka yangu.
10. Nimeipata barua pepe aliyonitumia Kamana.
18.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, tazameni picha hizi kisha mzijadilina kuziambatanisha na sentensi zilizo hapo chini kwa usahihi.

1. Barua pepe ya rais wa Marekani ina jumbe nyingi sana.
2. Watisapu yangu ina jumbe nyingi sana.
3. Barua pepe niliyomtumia mwalimu mkuu haijajibiwa.
4. Ninataka kufungua akaunti yangu ya fesibuku.Zoezi la makundi
Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, jadilini kuhusu umuhimu wa
tarakilishi kwa kuwaeleza wenzako:
1. Maana ya tarakilishi.
2. Njia za mawasiliano kupitia tarakilishi unazozifahamu.
3. Faida za tarakilishi kwa watumizi.4. Madhara ya tarakilishi kwa watumizi.
18.4 Kusikiliza na kuzungumza: Majadiliano
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu kuhusu
matumizi ya tarakilishi kisha mjadili kuhusu:
1. Faida za mradi wa tarakilishi kwa kila mtoto nchini Rwanda.
2. Kasoro za mradi wa tarakilishi kwa kila mtoto.
3. Mapendekezo yako kuhusiana na namna ya kuuboresha mradi huu.
4. Nchi nyingine ambazo zimewahi kutekeleza mradi huu wa tarakilishi kwa
kila mtoto.
5. Madhara na umuhimu wa kutumia:a) Fesibuku18.5 Sarufi
b) Barua pepech) Watisapu
Hali ya kuomba, tungo kanushi
A. Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, chunguzeni sentensi zinazofuata
kisha mwelezane ugunduzi wenu.1. Naomba uitoe simu hiyo kwenye chaji.B. Katika makundi yenu, chunguzeni sentensi zinazofuata kisha mwelezane
2. Tafadhali iwashe tarakilishi hiyo.
3. Tafadhali nunua mfuko wa kubebea tarakilishi yako.
4. Tafadhali naomba uniazime kitabu chako.5. Naomba uniletee kalamu hiyo
ugunduzi wenu.1. Naomba usiitoe simu hiyo kwenye chaji.
2. Tafadhali usiiwashe tarakilishi hiyo.
3. Tafadhali usinunue mfuko wa kubebea tarakilishi yako.
4. Tafadhali usiniazime kitabu chako.
5. Naomba usiniletee kalamu hiyo.
5. Naomba usiniletee kalamu hiyo.Je, mmegundua nini?
Maelezo muhimu!Tarakilishi i ni chombo cha mawasiliano mbacho hufanana na runinga
na hutuia iteaneti. Tarikiishi huhifadhi na kuchanganua taarifa
zilizongizwa pamoja na kuongoza mitambo mbalimbali.
Zoezi la 18.2
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwa
kutumia msamiati wa teknolojia ufuatao katika hali ya kuomba, tungo kanushi.
Kwa mfano: Tafadhali usiharibu tarakilishi ya baba.
1. Mtandao
2. Simu ya mkono
3. Intaneti
4. Kompyuta
5. Televisheni
6. Fesibuku
7. Watisapu
8. Baruapepe
Zoezi la 18.3
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, badilisheni sentensi zifuatazo
kutoka katika hali ya kuomba yakinishi hadi katika hali ya kuomba kanushi.
Kwa mfano: Naomba unipigie simu usiku.
Jibu: Naomba usinipigie simu usiku.
1. Tafadhali nunua televisheni nyingine.
2. Naomba unitengenezee simu yangu.
3. Naomba uninunulie bandali za intaneti.
4. Tafadhali mtoto huyo atumie tarakilishi yangu.5. Naomba uniandikie baruapepe kesho asubuhi.
SOMO LA 19: Redio na runinga
19.1 Kifungu kuhusu matumizi ya redio na runinga
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni mchoro na picha
zifuatazo kisha mjadili kuihusu. Baadaye, msome kifungu kilicho hapo chinikuhusu matumizi ya redio na runinga na mjibu maswali yanayofuata.


Maswali ya ufahamu
1. Eleza umuhimu wa redio na runinga kwa binadamu.
2. Redio na runinga hufundisha lugha na fasihi kwa njia gani?
3. Taja mifano mitatu ya msamiati wa redio na runinga.
4. Habari za kimataifa ni habari gani?
5. Taja mifano ya matangazo katika redio na runinga.
6. Ni kazi gani ya mtangazaji kulingana na kifungu ulichosoma?
7. Eleza maana ya ‘msikilizaji’ na ‘mtazamaji’ kwa kurejelea kifungu
ulichosoma.
8. Taja vituo vya redio na runinga unavyovijua nchini mwako.
9. Eleza madhara ya redio na runinga kwa binadamu.10. Eleza tofauti iliyopo kati ya redio na runinga.
19.2 Msamiati kuhusu matumizi ya redio na runinga
Kutokana na kifungu cha habari mlichosoma hapo awali, katika makundi ya
wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu maana ya msamiati mpya uliojitokeza
na unaohusiana na matumizi ya redio na runinga. Kamusi ya Kiswahili inawezakutumika panapohitajika.
Kwa mfano:
redio: chombo kinachopokea mawimbi ya sauti kutoka hewani ili mtuasikie habari, ujumbe au muziki unaochezwa kupitia kituo cha redio
Zoezi la 19.1
A. Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mchunguze
maana ya msamiati uliopigiwa mstari katika sentensi hizi. Tumieni kamusi
inapohitajika.1. Watu wengi wanapenda kutazama runinga.
2. Baba anasikiliza habari za kisiasa kwenye redio Rwanda.
3. Taarifa za habari zimepeperushwa hewani kwa wasikilizaji na
watazamaji.
4. Kaka yangu ni mtangazaji katika kituo cha runinga cha Rwanda.
5. Mawimbi ya sauti katika redio yetu yanasikika vizuri.
6. Matangazo ya biashara yameshakamilika.
7. Hawa ni watazamaji wa filamu ya watoto kwenye runinga.
8. Mkuu wa redio katika kituo chao ametuzwa.
9. Mimi ninapenda kutazama vipindi mbalimbali kwenye runinga.
B. Katika makundi yenu, tungeni sentensi sahihi kwa kutumia manenoyaliyopigiwa mistari katika sentensi za Zoezi la kwanza A.
19.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mjadili kuhusumatumizi ya redio na runinga kwa kuwaeleza wenzako:
1. Vipindi ambavyo unapenda kutazama kwenye runinga.
2. Vipindi ambavyo unapenda kusikiliza kwenye redio.
3. Mafunzo unayoyapata kutokana na vipindi unavyopenda kutazama na
kusikiliza.
4. Watangazaji unaowapenda kwenye runinga na sababu za kuwapenda.
5. Watangazaji unaowapenda kwenye redio na sababu za kuwapenda.619.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
Katika makundi ya wanafunzi watano watano, igizeni namna ya kutangaza
habari au vipindi mbalimbali kwenye runinga na redio. Mzingatie lugha ya
Kiswahili sanifu.
19.5 Sarufi: Hali ya kuamrisha, tungo yakinishi
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
kwa kuzisoma kwa sauti kisha mwelezane ugunduzi wenu.
1. Imba wimbo wa taifa.
2. Cheza mpira wa miguu.
3. Nenda usome kitabu hiki.
4. Pika muhogo kwa kuku.
5. Zungumza Kiswahili sanifu pekee.
Je, mmegundua nini?. Madhara ya redio na runinga kwa binadamu.

19.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
Katika makundi ya wanafunzi watano watano, igizeni namna ya kutangaza
habari au vipindi mbalimbali kwenye runinga na redio. Mzingatie lugha ya
Kiswahili sanifu.19.5 Sarufi: Hali ya kuamrisha, tungo yakinishi
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
kwa kuzisoma kwa sauti kisha mwelezane ugunduzi wenu.
1. Imba wimbo wa taifa.
2. Cheza mpira wa miguu.
3. Nenda usome kitabu hiki.
4. Pika muhogo kwa kuku.5. Zungumza Kiswahili sanifu pekee.
Je, mmegundua nini?
Maelezo muhimu!
Kitendo cha kutoa maagizo ya kufanyika kwa tendo fulani huitwa
kuamrisha.
Kwa mfano:
1. Nenda ukalale!
Katika sentensi hii, kuna agizo la mzungumziwa kwenda kulala.
2. Njoo hapa!
Katika sentensi hii, kuna agizo la mzungumziwa kwenda alikomzungumzaji.
Zoezi la 19.3
Tungeni sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo kwa njia ya kuamrisha
katika hali yakinishi.
Kwa mfano: washa (televisheni)
Jibu: Nenda uiwashe televisheni ile.
1. Andika (baruapepe)
2. Tengeneza (tarakilishi)
3. Jibu (simu)
4. Tuma (arafa)
5. Fundisha (teknolojia)
6. Sikiliza (redio)
7. Tazama (runinga)
8. Soma (fesibuku)
9. Fungua (watisapu)
10. Nunua (gazeti)
SOMO LA 20: Barua kwa mhariri20.1 Kifungu kuhusu barua kwa mhariri
Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni mchoro na picha
zifuatazo kisha mwelezane mnachokiona. Baadaye, msome kifungu kilicho hapo
chini na mjibu maswali yanayofuata.

