• Topic 5

    MADA KUU 5: LUGHA NA TEKNOLOJIA
    Mada Ndogo: Kiswahili katika teknolojia ya habari na

                                  mawasiliano.

    SOMO LA 17: Simu ya mkononi

    17.1 Mazungumzo kuhusu matumizi ya simu ya mkononi
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni picha zifuatazo
    kisha mwelezane vifaa mnavyoona pamoja na matumizi na umuhimu wake.
    Baadaye, msome kifungu cha mazungumzo kilicho hapo chini na mjibu maswali

    yanayofuata. 


                 

    Maswali ya ufahamu
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu cha
    mazungumzo yaliyo hapo juu kisha mjibu maswali yanayofuata.

    1. Taja wazungumzaji katika kifungu cha mazungumzo ulichosoma hapo
    juu.
    2. Bila shaka mazungumzo yanahusiana na teknolojia. Kwa nini? Eleza.
    3. Taja chombo cha mawasiliano kilichozungumziwa.
    4. Orodhesha matumizi yoyote mawili ya simu ya mkononi waliyotaja
    wazungumzaji.
    5. Mama ana matatizo gani kuhusiana na simu yake mpya?
    6. Kulingana na baba, ni mambo gani ambayo huathiri matumizi ya simu ya
    mkononi kijijini kwao?
    7. Teknolojia ni nini? Eleza kwa maneno yako mwenyewe.
    8. Taja msamiati wa adabu ambao umetumika katika kifungu cha

    mazungumzo mliyoyasoma.

    17.2 Msamiati kuhusu simu ya mkononi

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tafuteni msamiati mpya kutoka
    katika kifungu cha mazungumzo mlichosoma na kuueleza. Zingatieni matumizi
    ya msamiati huo katika kifungu hicho na mtumie kamusi pale inapohitajika.

    Zoezi la 17.1
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zifuatazo
    kisha mtunge sentensi sahihi kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mstari.

    1. Simu ya mkononi ambayo mama alinunuliwa inamsaidia sana.
    2. Teknolojia katika nchi yetu imekua kwa kiwango kikubwa.
    3. Simu ya babu yangu ni ya kubofya vidude.
    4. Dada yangu aliye ng’ambo alinitumia arafa kwenye simu yangu.
    5. Baba atampigia mwalimu wetu simu ili kuniombea ruhusa.
    6. Simu mpya aliyonayo ni ya kugusa kwenye kiwambo chake.
    7. Simu yangu ina kamera nzuri sana.

    8. Intaneti ni muhimu sana katika matumizi ya simu.

    Zoezi la 17.2

    Katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, kamilisheni sentensi zifuatazo
    kwa kutumia maneno yafuatayo:
    arafa, watisapu, kunasia mawimbi, fesibuku, simu, chaji
    Kwa mfano: Baba alinunua ____________ mpya baada ya ile ya
     kwanza kuibwa.
    Jibu:           Baba alinunua simu mpya baada ya ile ya kwanza kuibwa.
    1. Sharti simu iwe na ______________ ili iweze kutumika.
    2. Watu wengi siku hizi wanatumia _____________ na ______________
    kuwasiliana.
    3. Mitambo ya ____________ katika kijiji chetu imeharibika.
    4. Kaka alinitumia __________________ kunijulisha kuhusu gari jipya 
    alilonunua.

    17.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni mchoro na picha
    zifuatazo kisha mwelezane kinachoendelea kwa kurejelea:
    i) Vifaa vya mawasiliano unavyoviona;
    ii) Matumizi ya kila kifaa cha mawasiliano unachokiona;
    iii) Umuhimu wa kila kifaa cha mawasiliano unachokiona;
    iv) Kasoro au udhaifu wa kila kifaa cha mawasiliano unachokiona.
    

    Maelezo muhimu!
    Kifaa cha kutuma taarifa kwa njia ya kielektroniki kwa kutumia simu
    huitwa faksi. Taarifa inayotumwa pia huitwa faksi. Huhusisha matumizi
    ya umeme. Faksi ni aina ya barua au ujumbe unaotumwa kwa njia ya
    mashine inayoitwa faksi. Maelezo machache yanayofafanua ujumbe
    pekee hutumika.


    17.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo
    Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, igizeni mazungumzo mliyosoma
    hapo juu kati ya Baba na Mama.

    17.5 Sarufi

    Hali ya kuomba, tungo yakinishi

    A. Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
    kisha mwelezane ugunduzi wenu na baadaye mjibu zoezi l7.3 linalofuata.

    1. Tafadhali nipigie simu unapofika nyumbani.
    2. Tafadhali imba wimbo wa taifa.
    3. Tafadhali cheza mpira wa miguu.
    4. Tafadhali pikeni mihogo kwa kuku.
    5. Tafadhali zungumza lugha ya Kiswahili sanifu pekee.

    B. Badilisheni sentensi mlizosoma hapo juu kwa kutumia ‘naomba’.

    Maelezo muhimu!

    Msamiati wa adabu ambao hutumika kuomba mtu akutendee hisani

    fulani ni kama vile: tafadhali, naomba, n.k.

    Zoezi la 17.3

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi tano sahihi

    katika hali ya kuomba, wakati uliopo.

    SOMO LA 18: Matumizi ya tarakilishi

    18.1 Kifungu kuhusu matumizi ya tarakilishi

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu mnachokiona
    katika mchoro na picha ifuatayo na mwelezane maana na matumizi yake.
    Baada ya hapo, msome kifungu cha habari kilicho hapo chini na mjibu maswali

    yanayofuata.


    Maswali ya ufahamu
    1. Taja faida zozote mbili za mradi wa tarakilishi kwa wanafunzi.
    2. Taja faida zozote mbili za tarakilishi kwa watu kwa ujumla.
    3. Jina jingine la tarakilishi ni lipi?
    4. Mtandao hufanya ulimwengu kuwa kama kijiji kimoja. Kweli au la? Kivipi?
    Eleza.
    5. Jadili upungufu mkubwa wa watisapu kulingana na kifungu ulichosoma.
    6. Pendekeza anwani nyingine mwafaka kwa taarifa hii.
    7. Je, teknolojia ina manufaa gani kwa nchi? Taja manufaa matano.
    8. Eleza madhara yanayoweza kusababishwa na tarakilishi.
    9. Matumizi ya tarakilishi yanawezesha vipi utangamano wa wanajamii
    mbalimbali?
    10. Jadili matumizi, umuhimu na madhara ya:

    a) Fesibuku                             b) Watisapu            ch) Barua pepe

    18.2 Msamiati kuhusu matumizi ya tarakilishi

    Jipangeni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mtafute maana
    ya msamiati mpya katika kifungu mlichosoma hapo awali. Tafuteni maana ya
    msamiati huo kulingana na matumizi yake katika kifungu hicho. Tumieni kamusi

    pale inapohitajika. 

    Zoezi la 18.1
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi hizi kisha
    mtunge sentensi zenu kwa kutumia maneno yaliyopigiwa mistari.

    1. Teknolojia imeufanya ulimwengu kuwa kama kijiji kidogo.
    2. Tarakilishi ina manufaa mengi kwa binadamu.
    3. Mtandao humwezesha mtafiti kupata taarifa nyingi.
    4. Mradi wa tarakilishi kwa kila mwanafunzi utafaulu.
    5. Mimi huisoma kamusi ya Kiswahili kwenye tarakilishi.
    6. Tunaweza kuzifahamu tamaduni za jamii jirani kupitia kwa mtandao.
    7. Wanajamii mbalimbali hutangamana kupitia kwa mtandao.
    8. Akaunti yangu ya fesibuku imefungwa.
    9. Watisapu yangu imejaa picha tele za harusi ya kaka yangu.
    10. Nimeipata barua pepe aliyonitumia Kamana. 

    18.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
    Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, tazameni picha hizi kisha mzijadili

    na kuziambatanisha na sentensi zilizo hapo chini kwa usahihi. 


    1. Barua pepe ya rais wa Marekani ina jumbe nyingi sana.
    2. Watisapu yangu ina jumbe nyingi sana.
    3. Barua pepe niliyomtumia mwalimu mkuu haijajibiwa.
    4. Ninataka kufungua akaunti yangu ya fesibuku. 

    Zoezi la makundi 

    Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, jadilini kuhusu umuhimu wa
    tarakilishi kwa kuwaeleza wenzako:
    1. Maana ya tarakilishi.
    2. Njia za mawasiliano kupitia tarakilishi unazozifahamu.
    3. Faida za tarakilishi kwa watumizi.

    4. Madhara ya tarakilishi kwa watumizi.

    18.4 Kusikiliza na kuzungumza: Majadiliano

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, someni tena kifungu kuhusu
    matumizi ya tarakilishi kisha mjadili kuhusu:
    1. Faida za mradi wa tarakilishi kwa kila mtoto nchini Rwanda.
    2. Kasoro za mradi wa tarakilishi kwa kila mtoto.
    3. Mapendekezo yako kuhusiana na namna ya kuuboresha mradi huu.
    4. Nchi nyingine ambazo zimewahi kutekeleza mradi huu wa tarakilishi kwa
    kila mtoto.
    5. Madhara na umuhimu wa kutumia:
    a) Fesibuku
    b) Barua pepe

    ch) Watisapu

    18.5 Sarufi
    Hali ya kuomba, tungo kanushi
    A. Katika makundi ya wanafunzi wanne wanne, chunguzeni sentensi zinazofuata
    kisha mwelezane ugunduzi wenu.
    1. Naomba uitoe simu hiyo kwenye chaji.
    2. Tafadhali iwashe tarakilishi hiyo.
    3. Tafadhali nunua mfuko wa kubebea tarakilishi yako.
    4. Tafadhali naomba uniazime kitabu chako.

    5. Naomba uniletee kalamu hiyo

    B. Katika makundi yenu, chunguzeni sentensi zinazofuata kisha mwelezane
    ugunduzi wenu.

    1. Naomba usiitoe simu hiyo kwenye chaji.
    2. Tafadhali usiiwashe tarakilishi hiyo.
    3. Tafadhali usinunue mfuko wa kubebea tarakilishi yako.
    4. Tafadhali usiniazime kitabu chako.
    5. Naomba usiniletee kalamu hiyo.
    5. Naomba usiniletee kalamu hiyo.

    Je, mmegundua nini?

    Maelezo muhimu!

    Tarakilishi  i ni chombo cha mawasiliano mbacho hufanana na runinga

    na hutuia iteaneti. Tarikiishi huhifadhi na kuchanganua taarifa

    zilizongizwa pamoja na kuongoza mitambo mbalimbali.


    Zoezi la 18.2


    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tungeni sentensi sahihi kwa
    kutumia msamiati wa teknolojia ufuatao katika hali ya kuomba, tungo kanushi.
    Kwa mfano:                    Tafadhali usiharibu tarakilishi ya baba.
    1. Mtandao
    2. Simu ya mkono
    3. Intaneti
    4. Kompyuta
    5. Televisheni
    6. Fesibuku
    7. Watisapu
    8. Baruapepe

    Zoezi la 18.3
    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, badilisheni sentensi zifuatazo
    kutoka katika hali ya kuomba yakinishi hadi katika hali ya kuomba kanushi.
    Kwa mfano: Naomba unipigie simu usiku.
    Jibu:        Naomba usinipigie simu usiku.
    1. Tafadhali nunua televisheni nyingine.
    2. Naomba unitengenezee simu yangu.
    3. Naomba uninunulie bandali za intaneti.
    4. Tafadhali mtoto huyo atumie tarakilishi yangu.

    5. Naomba uniandikie baruapepe kesho asubuhi.

    SOMO LA 19: Redio na runinga

    19.1 Kifungu kuhusu matumizi ya redio na runinga

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni mchoro na picha
    zifuatazo kisha mjadili kuihusu. Baadaye, msome kifungu kilicho hapo chini

    kuhusu matumizi ya redio na runinga na mjibu maswali yanayofuata.




     

    Maswali ya ufahamu
    1. Eleza umuhimu wa redio na runinga kwa binadamu.
    2. Redio na runinga hufundisha lugha na fasihi kwa njia gani?
    3. Taja mifano mitatu ya msamiati wa redio na runinga.
    4. Habari za kimataifa ni habari gani?
    5. Taja mifano ya matangazo katika redio na runinga.
    6. Ni kazi gani ya mtangazaji kulingana na kifungu ulichosoma?
    7. Eleza maana ya ‘msikilizaji’ na ‘mtazamaji’ kwa kurejelea kifungu
    ulichosoma.
    8. Taja vituo vya redio na runinga unavyovijua nchini mwako.
    9. Eleza madhara ya redio na runinga kwa binadamu.

    10. Eleza tofauti iliyopo kati ya redio na runinga.

    19.2 Msamiati kuhusu matumizi ya redio na runinga

    Kutokana na kifungu cha habari mlichosoma hapo awali, katika makundi ya
    wanafunzi watatu watatu, jadilini kuhusu maana ya msamiati mpya uliojitokeza
    na unaohusiana na matumizi ya redio na runinga. Kamusi ya Kiswahili inaweza

    kutumika panapohitajika.

    Kwa mfano:

    redio: chombo kinachopokea mawimbi ya sauti kutoka hewani ili mtu

    asikie habari, ujumbe au muziki unaochezwa kupitia kituo cha redio

    Zoezi la 19.1

    A. Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watatu watatu kisha mchunguze
    maana ya msamiati uliopigiwa mstari katika sentensi hizi. Tumieni kamusi
    inapohitajika.
    1. Watu wengi wanapenda kutazama runinga.
    2. Baba anasikiliza habari za kisiasa kwenye redio Rwanda.
    3. Taarifa za habari zimepeperushwa hewani kwa wasikilizaji na
    watazamaji.
    4. Kaka yangu ni mtangazaji katika kituo cha runinga cha Rwanda.
    5. Mawimbi ya sauti katika redio yetu yanasikika vizuri.
    6. Matangazo ya biashara yameshakamilika.
    7. Hawa ni watazamaji wa filamu ya watoto kwenye runinga.
    8. Mkuu wa redio katika kituo chao ametuzwa.
    9. Mimi ninapenda kutazama vipindi mbalimbali kwenye runinga.
    B. Katika makundi yenu, tungeni sentensi sahihi kwa kutumia maneno

    yaliyopigiwa mistari katika sentensi za Zoezi la kwanza A.

    19.3 Matumizi ya lugha: Majadiliano
    Jigaweni katika makundi ya wanafunzi watano watano kisha mjadili kuhusu

    matumizi ya redio na runinga kwa kuwaeleza wenzako:

    1. Vipindi ambavyo unapenda kutazama kwenye runinga.
    2. Vipindi ambavyo unapenda kusikiliza kwenye redio.
    3. Mafunzo unayoyapata kutokana na vipindi unavyopenda kutazama na
    kusikiliza.
    4. Watangazaji unaowapenda kwenye runinga na sababu za kuwapenda.
    5. Watangazaji unaowapenda kwenye redio na sababu za kuwapenda.

     619.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo

    Katika makundi ya wanafunzi watano watano, igizeni namna ya kutangaza

    habari au vipindi mbalimbali kwenye runinga na redio. Mzingatie lugha ya

    Kiswahili sanifu.

    19.5 Sarufi: Hali ya kuamrisha, tungo yakinishi

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata

    kwa kuzisoma kwa sauti kisha mwelezane ugunduzi wenu.

    1. Imba wimbo wa taifa.

    2. Cheza mpira wa miguu.

    3. Nenda usome kitabu hiki.

    4. Pika muhogo kwa kuku.

    5. Zungumza Kiswahili sanifu pekee.

    Je, mmegundua nini?. Madhara ya redio na runinga kwa binadamu.

    19.4 Kusikiliza na kuzungumza: Maigizo

    Katika makundi ya wanafunzi watano watano, igizeni namna ya kutangaza
    habari au vipindi mbalimbali kwenye runinga na redio. Mzingatie lugha ya
    Kiswahili sanifu.
    19.5 Sarufi: Hali ya kuamrisha, tungo yakinishi

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, chunguzeni sentensi zinazofuata
    kwa kuzisoma kwa sauti kisha mwelezane ugunduzi wenu.

    1. Imba wimbo wa taifa.
    2. Cheza mpira wa miguu.
    3. Nenda usome kitabu hiki.
    4. Pika muhogo kwa kuku.

    5. Zungumza Kiswahili sanifu pekee.

    Je, mmegundua nini?

    Maelezo muhimu!

    Kitendo cha kutoa maagizo ya kufanyika kwa tendo fulani huitwa
    kuamrisha.
    Kwa mfano:
    1. Nenda ukalale!
    Katika sentensi hii, kuna agizo la mzungumziwa kwenda kulala.
    2. Njoo hapa!
    Katika sentensi hii, kuna agizo la mzungumziwa kwenda aliko

    mzungumzaji.

    Zoezi la 19.3

    Tungeni sentensi sahihi kwa kutumia maneno yafuatayo kwa njia ya kuamrisha
    katika hali yakinishi.

    Kwa mfano: washa (televisheni)
    Jibu:                Nenda uiwashe televisheni ile.
    1. Andika (baruapepe)
    2. Tengeneza (tarakilishi)
    3. Jibu (simu)
    4. Tuma (arafa)
    5. Fundisha (teknolojia)
    6. Sikiliza (redio)
    7. Tazama (runinga)
    8. Soma (fesibuku)
    9. Fungua (watisapu)
    10. Nunua (gazeti)

    SOMO LA 20: Barua kwa mhariri

    20.1 Kifungu kuhusu barua kwa mhariri

    Katika makundi ya wanafunzi watatu watatu, tazameni mchoro na picha
    zifuatazo kisha mwelezane mnachokiona. Baadaye, msome kifungu kilicho hapo
    chini na mjibu maswali yanayofuata. 

    SURA NINE: MADA KUU 4: UIMARISHAJI WA STADI YA UANDISHI NA MASIMULIZI KUPITIA LUGHA YA KISWAHILITopic 6